Hapa Kazi Tu...JPM Aweka Rekodi ya Siku 25 bila Baraza la Mawaziri

Rais John Pombe Magufuli amekuwa wa kwanza tangu mfumo wa vyama vingi kuanza nchini kutumia muda mrefu kutangaza Baraza la Mawazi kutok...


Rais John Pombe Magufuli amekuwa wa kwanza tangu mfumo wa vyama vingi kuanza nchini kutumia muda mrefu kutangaza Baraza la Mawazi kutokana na kile wasomi, wachambuzi wa siasa kusema pengine anapata wakati mgumu kupata mawaziri watakaoendana na kasi yake.

Katiba ya mwaka 1977 inamtaka Rais kumteua waziri mkuu ndani ya siku 14 tangu alipoapishwa na kulipeleka jina lake bungeni, lakini katiba hiyo ipo kimya kuhusu uteuzi wa mawaziri, hivyo Rais anaweza kutumia muda wowote.

Wakati Rais mstaafu, Benjamin Mkapa alipoingia madarakani mwaka 1995 aliteua baraza la mawaziri Novemba 28, siku tano baada ya kuapishwa, Jakaya Kikwete alitangaza Baraza la kwanza Siku 14 baada ya kuapishwa na Dk Magufuli hadi sasa, siku 25 zimepita tangu aapishwe Novemba 5, mwaka huu hajafanya hivyo.

Kazi ambazo Rais Magufuli ameanza kuzifanya bila mawaziri ni kuzuia safari za nje, kuzuia sherehe za Uhuru na kuanza kupambana na wabadhirifu wa fedha za umma.

 Wasomi hao wakilinganisha alichokisema kwenye hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge, walisema kuwa ana njozi za Tanzania aitakayo huku akieleza wazi kuwa anatambua kuna mawaziri, wabunge wanakula rushwa na akibainisha wazi hana imani kama waliomo ndani ya CCM wanakula pia.


Mhadhiri wa Idara ya Sayansi ya Siasa, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Richard Mbunda, alisema kwenye mitandao ya kijamii kuna utani unazunguka kuwa kwa kasi yake anaweza kufanya kazi hata bila kuwa na mawaziri.

“Ni utani, lakini ukiuchunguza mara mbili unaona kabisa hata wananchi wameona anachokifanya na wanahitaji kukiona hicho kutoka kwenye Baraza lake,” alisema. Alisema kasi yake na kubana matumizi alikoanza nako anahitaji kuwa makini kwa sababu alitamka anataka kuwa na baraza dogo la mawaziri.


Alifafanua kuwa kwenye Serikali ya Awamu ya Nne mwaka 2005, mawaziri na naibu wao idadi yao ilikaribia 60, wakitumia mashangingi yanayokula mafuta, posho, hivyo ili kudhibiti hilo atachukua muda pia, ikiwamo kuvunja baadhi ya wizara kama ataona itafaa na kumsaidia anachotaka kukifanya.

Related

Siasa 966361453961112945

Post a Comment

emo-but-icon

item