Taarifa ya Upotevu wa Makontena Azam ICD Toka SSB Group of Companies
Kumekua na taarifa zinazosamabazwa katika mitandao ya kijamii kuwa Kapuni ya Bakhresa inahusika na upotevu wa Makontena 349 yaliyolipo...
http://taarifayahabari360.blogspot.com/2015/11/taarifa-ya-upotevu-wa-makontena-azam.html
Kumekua na taarifa zinazosamabazwa katika mitandao ya
kijamii kuwa Kapuni ya Bakhresa inahusika na upotevu wa Makontena 349 yaliyolipotiwa
hivi karibuni kuwa yametolewa bandarini bila kulipiwa ushuru.Taarifa hizo
zilitolewa na Waziri Mkuu wakati wa ziara yake Bandari ya Dar es salaam hivi
karibuni.
Uchunguzi wetu umeonyesha kuwa sio kweli kuwa kuna
makontena yenye bidhaa zilizoingizwa na kampuni hiyo ama ni miongoni mwa
makontena yaliyohusika na sakata hilo.Isipokua kumetokea upotevu wa makontena
yaliyoingizwa nchini na baadhi ya
wafanyabiashara katika eneo la kuhifadhia makontena (ICD) linalomilikiwa na
kampuni hiyo ya Azam ICD.
Aidha imebainika kuwa kuna uchunguzi unaofanywa na
mamlaka ya mapato nchini TRA, huku kukiwa na ushirikiano na uongozi wa Kamapuni
hiyo (SSB Group of Companies) kuhakikisha wale wote wanaohusika upotevu huo
wanachukuliwa hatua na kodi yote ya serikali inalipwa na wamiliki wote wa
makontena yaliyohusika katika upotevu huo wanawajibishwa.
SSB Group of Companies
Corporate Affairs Department
November 29 ,2015
