MSD yakarabati jengo la duka la dawa hospitali ya taifa Muhimbili
BOHARI ya Dawa (MSD) imejiimarisha na kuhahikisha inatekeleza kwa wakati agizo la Rais Dk. John Magufuli la kuweka maduka ya dawa katik...
http://taarifayahabari360.blogspot.com/2015/11/msd-yakarabati-jengo-la-duka-la-dawa.html
BOHARI ya Dawa (MSD) imejiimarisha na kuhahikisha
inatekeleza kwa wakati agizo la Rais Dk. John Magufuli la kuweka maduka ya dawa
katika hospitali za rufaa na kanda nchini.
Katika kutekeleza agizo hilo MSD imeanza kwa kasi kubwa
ya kukarabati jengo la duka la dawa katika Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili (MNH), ambalo linatarajiwa kufunguliwa kesho.
Mwandishi wa habari hii alishuhudia jana kasi kubwa ya
mafundi ujenzi wakikarabati jengo hilo ambalo awali lilikuwa likitumika
kama stoo ya kuhifadhi vitu mbalimbali vya hospitali hiyo.
Akizungumza na vyombo vya habari hivi karibuni kuhusu
ufunguzi wa maduka hayo, Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laureane Bwanakunu
alisema agizo la Rais la kuitaka MSD kuanzisha duka la dawa karibu na
hospitali limekuja wakati muafaka kwani kwenye mpango mkakati wa miaka
sita wa MSD tayari ilikuwa na mpango wa kufungua maduka hayo kwa ajili ya
kusogeza huduma karibu a wananchi.
Alisema maduka ya MSD ambayo yatafunguliwa kwenye
hospitali za rufaa na kanda yatafanya kazi masaa 24 na kuuza dawa na vifaa tiba
chini ya bei ya soko pia yatahudumia watu binafsi na wale waliopo kwenye
taratibu za Bima ya afya kote nchini.
“Ili kudhibiti watumishi wasio waaminifu kuiba dawa MSD
inafanya kazi za uagizaji, uhifadhi na usambazaji kwa kutumia mfumo wa
mtandao wa E9 na tangu mwaka wa fedha uliopita tumeanza kuziwekea alama ya GOT
bidhaa zetu ikiwa ni pamoja na vidonge.” alisema Bwanakunu.
Alisema vidonge ambavyo tayari vimewekewa nembo ya GOT
vipo 45 na wanaendelea kuwapa maelekezo wazabuni ili vyote viwekwe alama
hizo..,nembo ya serikali inaonekana kwenye dawa za serikali kama Diclofenac,
moxillin, iprofloxacin, Contrimoxale,paracetamol,na magnesium.
Alisema wanatarajia kuanzisha huduma ya kutoa taarifa kwa
njia ya simu pale wananchi watakapoona kuna wizi wa dawa za serikali na kwamba
wananchi wanaelimishwa kutoa taarifa pale wanapoona dawa za serikali
mitaani.
Alisema, pamoja na serikali kuanza kupunguza deni lake linalodaiwa
na MSD bado inadaiwa Sh.bilioni 53.