Gesi Inayozalishwa MADIMBA Mtwara Yatumika Chini ya Uzalishaji wake
Serikali imeshauriwa kuharakishakuongeza uzalishaji katika mitambo ya kuchakata na kusambaza gesi ya MADIMBA mkoani MTWARA ili wananchi...
http://taarifayahabari360.blogspot.com/2015/12/gesi-inayozalishwa-madimba-mtwara.html
Serikali imeshauriwa kuharakishakuongeza uzalishaji
katika mitambo ya kuchakata na kusambaza gesi ya MADIMBA mkoani MTWARA ili
wananchi waweze kuondokana na kero ya kukatika kwa umeme pamoja na kuibua fursa
za uanzishwaji wa viwanda vingine
Hayo yameelezwa na wadau wa masuala ya gesi baada ya
kutembelea katika mradi wa gesi asilia uliopo MADIMBA na
kuelezwa kuwa kati ya
gesi yote inayozalishwa eneo hilo ni chini ya robo ndio inayochukuliwa na
TANESCO kwa ajili ya kuzalisha umeme wa KINYEREZI huku gesi nyingine ikibaki
bila matumizi yeyote kwa sasa hali inayopelekea mtambo mmoja tuu kutumika kati
ya mitambo mitatu iliyopo.
Mkufunzi wa masuala ya mafuta na gesi DEO MFUGALE amesema
serikali inatakiwa kuhakikisha inaitumia mitambo yote mitatu iliyopo katika
eneo la MADIMBA badala ya kutumia mtambo mmoja pekee.
Katika hatua nyingine uwepo wa mradi huu katika eneo la
MADIMBA umewanufaisha wakazi wa vijiji vya jirani wanaonufaika na huduma ya
maji safi na salama inayotolewa bure
