Gary Neville ateuliwa kuwa kocha mkuu wa Valencia

Beki wa zamani wa Manchester United na kocha wa kikosi cha kwanza cha timu ya taifa Wingereza, Gary Neville ameteuliwa kuwa kocha mku...



Beki wa zamani wa Manchester United na kocha wa kikosi cha kwanza cha timu ya taifa Wingereza, Gary Neville ameteuliwa kuwa kocha mkuu wa klabu ya Valencia inayoshiriki Ligi kuu ya Hispania.
Gary Neville ameteuliwa kocha mkuu kwa mkataba mfupi na ataongoza timu hiyo mpaka mwishoni mwa msimu huu.

Neville amechukua nafasi hiyo baada ya siku chache zilizopita kutimuliwa kazi kwa aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo, Nuno Santo na sasa Gary Neville atafanya kazi na ndugu yake Phil Neville ambaye atakuwa msaidizi wake.

Akizungumzia kuteuliwa kwake, Neville amesema ni furaha kwake kupata nafasi katika timu hiyo na atatumia uwezo wake kuifikisha mbali timu hiyo na amekuwa akiifatilia kwa muda mrefu anafahamu nini wanahitaji.

“Nina furaha sana kuteuliwa kuwa kocha hapa, nimeifahamu Valencia tangu nikiwa nacheza mpira najua mashabiki wa timu hii wanahitaji vitu vizuri tutashirikiana pamoja kuweza kuisaidia timu kufika mbali ina kikosi vizuri nataraji tutafanya vizuri,” amesema Neville.

Nae Rais wa Valencia, Person Layhoon Chan amesema wamemteua Neville kwa kutambua uwezo wake na wanaimani ataifikisha timu yao mbali zaidi ya walipo sasa.

“Tuna furaha kumtambulisha Neville kama kocha wetu mkuu ataeongoza timu hadi mwishoni kwa msimu, tunatambua uwezo wake ni mzuri tunataraji mambo mazuri akishirikiana na wenzake waliopo katika kikosi chetu,” amesema Chan.

Neville ataanza kibarua chake siku ya Jumapili Desemba, 6 kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya UEFA dhidi ya Lyon ya Ufaransa katika Uwanja wa Mestalla siku ya Jumatano Desemba,9.


Related

Kitaifa 195822759860411909

Post a Comment

emo-but-icon

item