UKAWA Wapewa Ruksa Kuzindua Kampeni zao Jangwani Jumamosi Hii

Ruksa Kutumia Uwanja wa jangwani ya vyama vinavyounda UKAWA ya kukatazwa kutumia uwanja wa jangwani kuzindua kampeni yameanza kufanyiwa kazi...

Ruksa Kutumia Uwanja wa jangwani

ya vyama vinavyounda UKAWA ya kukatazwa kutumia uwanja wa jangwani kuzindua kampeni yameanza kufanyiwa kazi na tume ya taifa ya uchaguzi na  taarifa zilizotolewa na mkuu wa idara ya mawasiliano ya CHADEMA Bw.Tumaini Makene zimesema kuwa uzinduzi huo utafanyika kwenye uwanja huo kama ilivyokuwa imepangwa.

Bw.Makene ametoa taarifa hiyo kwenye mkutano wa baraza la vijana la vyama  vinavyounda UKAWA na waandishi wa habari ambao pia viongozi hao wametumia  nafasi hiyo kuiomba tume ya uchaguzi kuwakemea viongozi na watendaji wa  serikali kufanya kazi za siasa kwa lengo la kukibeba chama tawala.

Viongozi hao wa vijana wamesema  hatua ya viongozi na watendaji wa serikali ya kujihusisha moja kwa moja na kampeni za  CCM huku wengine wakitumia rasilimali za umma  na vyombo vya dola kukandamiza vyama vya upinzani inathibitisha ukweli wa  malalamiko yao.

Related

Uchaguzi Mkuu 2015 3220565073957608349

Post a Comment

emo-but-icon

item